ZOEZI LA UTOAJI ELIMU UNAENDELEA KWA WASAFIRISHAJI MKOANI MBEYA - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Monday 4 March 2019

ZOEZI LA UTOAJI ELIMU UNAENDELEA KWA WASAFIRISHAJI MKOANI MBEYA

Mkuu wa Kitengo cha Usalama na Mazingira kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Julius Chambo, akitoa elimu kwa madereva wa malori kuhusu utekelezaji wa Sheria mpya ya Udhibiti wa Uzito wa Magari ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, mjini Tunduma, mkoani Mbeya. Sheria hiyo imeshaanza kutumika tarehe 1 Machi, 2019.

Dereva wa malori ya mizigo Bw. Juma Nachikolo, akiuliza swali kwa Mkuu wa Kitengo cha Usalama na Mazingira kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Julius Chambo (hayupo pichani), mara baada ya kupewa elimu ya Sheria mpya ya Udhibiti wa Uzito wa Magari ya Jumuiya ya Afrika Mashariki iliyoanza kutumika tarehe 1 Machi, 2019, mjini Tunduma, mkoani Mbeya.

No comments:

Post a Comment