MTANGAZAJI MAARUFU KIBONDE 'AMFUATA' RUGE - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Thursday 7 March 2019

MTANGAZAJI MAARUFU KIBONDE 'AMFUATA' RUGE

Mtangazaji maarufu, Ephraim Kibonde 


IMEPITA siku tisa tangu kituo cha Utangazaji cha Clouds Media kupata pigo kwa kuondokewa na aliyekuwa Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa kituo hicho, Ruge Mutahaba, wamepata pigo jingine baada ya kuondokewa na mtangazaji wake maarufu, Ephraim Kibonde aliyekuwa akiendesha kipindi cha Jahazi. Kifo cha mtangazaji huyo kimetokea Machi 7, 2019.

Vyanzo vya habari vinaeleza kuwa Kibonde amefariki akiwa Mwanza na alianza kusumbuliwa na presha tangu akiwa Bukoba kwenye msiba wa Ruge na kulazimika kukimbizwa hospitali kabla ya kuhamishiwa jijini Mwanza alipo kubwa na mauti hayo. Mwana ametoa na ametwaa jina lake lihimidiwe. Apumzike kwa amani Kibonde. Amina

No comments:

Post a Comment