MUSSA ZUNGU ACHAGULIWA SPIKA BUNGE LA TANZANIA - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Tuesday, 11 November 2025

MUSSA ZUNGU ACHAGULIWA SPIKA BUNGE LA TANZANIA

 

MBUNGE wa Jimbo la Ilala jijini Dar es Salaam, Mussa Zungu, amechaguliwa kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Uchaguzi huo umefanyika jijini Dodoma ambapo Zungu amepata kura 378 zilizopigwa na wabunge na kumuwezesha kushika nafasi hiyo muhimu ya kuongoza Bunge la 13 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

 

Ushindi huo unampa jukumu la kusimamia shughuli zote za chombo hicho cha kutunga sheria, kuhakikisha uwajibikaji na kuimarisha utekelezaji wa majukumu ya Bunge kwa manufaa ya wananchi. Katika uchaguzi huo, wagombea wengine waliokuwa wakishindana naye ni Veronica Tyeah kutoka Chama cha National Reconstruction Alliance (NRA) aliyepata kura 0, Anitha Mgaya wa National League for Democracy (NLD) kura 0, Chrisant Nyakitita wa Democratic Party (DP) kura 0, Ndonge Ndonge wa Alliance for Africa Farms Party (AAFP) aliyepata kura 1, na Amin Yango wa Alliance for Democratic Change (ADC) aliyepata kura 1.


No comments:

Post a Comment