MBUNGE ASIA HALAMGA SASA RASMI KUWATUMIKIA WANANCHI HANANG' - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Wednesday, 12 November 2025

MBUNGE ASIA HALAMGA SASA RASMI KUWATUMIKIA WANANCHI HANANG'


Mbunge wa Jimbo la Hanang’ Mhe. Asia Halamga akila kiapo cha Utii na Uaminifu na kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kikao cha kwanza cha mkutano wa kwanza wa Bunge la 13,  leo Novemba 11, 2025 Jijini Dodoma.

Na Dotto Mwaibale, Dodoma 

MBUNGE Mteule wa Jimbo la Hanang’ kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Manyara Asia Halamga ameendelea kung’ara katika medani za siasa na kuwa gumzo katika mkoa huo na Tanzania kwa ujumla. 

Halamga ni mbunge msikivu, mnyenyekevu, mpole, mwenye maono na mpenda maendeleo ambaye amekuwa akiguswa na changamoto za wananchi pasipo ubaguzi. 

Nyota yake ya kisiasa ilianza kuchipuka kupitia Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) na hasa baada ya kugombea ubunge wa Vijana Taifa kupitia CCM ambapo alishinda kwa kupata kura za kutosha. 

Akiwa mbunge kupitia Vijana Halamga alifanya kazi kubwa nzuri ya kuwatumikia wananchi kwa nguvu zake zote liwake jua, inyeshe mvua alikuwa bega kwa bega na wananchi jambo lililomfanya aendelee kupendwa na nyota yake kung’ara. 

Uchaguzi Mkuu wa 2025,  Halamga aligombea Ubunge wa Jimbo la Hanang’ na katika kura za maoni ndani ya chama alishinda kwa kupata kura 7,092 na kuwashinda wagombea wenzake watano, akiwemo aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo hilo Dkt. Mary Nagu aliyepata kura 5,237.

Mary Nagu anatajwa kuweka rekodi ya kushika nafasi za Uwaziri katika wizara mbalimbali kwa muda mrefu. 

Uchaguzi huo wa kura za maoni ulihusisha wajumbe 21,094 na wajumbe 16,384 walijitokeza kushiriki zoezi hilo na matokeo ya kura Halamga aliibuka mshindi kwa kupata kura 7,092,  Mary Nagu – 5,237, Samwel Hhayuma 2,995, Franklin Sumaye 399,  John Lory 189 na Qambemeda Nyangura kura 152. 

Wahenga walisema nyota njema uonekana mapema asubuhi hivyo basi kwa ushindi huo alioupata ndani ya chama ulionesha safari ya mafanikio yake katika siasa kuelekea uchaguzi mkuu ambapo alishinda kwa kura nyingi. 

Tume  Huru ya Taifa ya uchaguzi (INEC) ilimtangaza Asia Halamga kuwa mshindi wa nafasi ya Ubunge Jimbo la Hanang’ kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).
‎Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Hanang, Geogrey Abayo alisema sia Halamga alipata kura 173,330 sawa na asilimia 99.3. 

Akitangaza matokeo katika kituo cha majumuisho ya kura ya Rais na mbunge ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang Oktoba 30, 2025 alibainisha kwamba wananchi waliojiandikisha kupiga kura ni 196,630,waliopiga kura ni 174,449 ambapo kura halali ni 173,343, ‎kura zilizokataliwa ni 1,106.
‎Aidha, mbunge Asia Halamga kama mgombea pekee alikabidhiwa hati ya ushindi na hati ya kuchaguliwa rasmi kuwa Mbunge wa Jimbo la Hanang.
‎Mbunge wa Jimbo la Hanang’ Asia Halamga Novemba 11, 2025 amekula kiapo cha Utii na Uaminifu na kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kikao cha kwanza cha mkutano wa kwanza wa Bunge la 13 na sasa yupo rasmi  kuwatumikia wana Hanang’ kwa kutekeleza ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2025/ 2030.

Mhe. Asia Halamga akikabidhiwa vitendea kazi.

No comments:

Post a Comment