JOKATE AWAPONGEZA ROOM TO REEAD KUCHOCHEA WANAFUNZI USOMAJI VITABU - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Tuesday, 14 October 2025

JOKATE AWAPONGEZA ROOM TO REEAD KUCHOCHEA WANAFUNZI USOMAJI VITABU

 

Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Jokate Mwegelo (wa pili kushoto) pamoja na Mkurugenzi wa Shirika la Room To Read- Tanzania, Bi. Joan Minja (wa tatu kulia) wakionesha nakala za kitabu cha  ‘She Creates Changes’ mara baada ya kuzinduliwa rasmi.

Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Jokate Mwegelo (wa pili kushoto) pamoja na Mkurugenzi wa Shirika la Room To Read- Tanzania, Bi. Joan Minja (wa tatu kulia) wakipiga makofi mara baada ya uzinduzi wa nakala za kitabu cha ‘She Creates Changes’.

Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Jokate Mwegelo (wa pili kushoto) pamoja na Mkurugenzi wa Shirika la Room To Read- Tanzania, Bi. Joan Minja (wa tatu kulia) wakikata utepe kuashiria uzinduzi wa nakala za kitabu cha ‘She Creates Changes’ kilichozinduliwa na.Shirika la Room To Read.

Sehemu ya washiriki wa uzinduzi wa nakala za kitabu cha ‘She Creates Changes’ kilichozinduliwa na.Shirika la Room To Read.

Sehemu ya wageni waalikwa na wanafunzi wakifuatilia matukio kwenye hafla ya uzinduzi wa nakala za kitabu cha ‘She Creates Changes’.

Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Jokate Mwegelo akizungumza kwenye maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Mtoto wa Kike yaliyoenda sambamba na uzinduzi wa Kitabu cha ‘She Creates Changes’ na video zinazoangazia mafanikio ya msichana aliyepitia changamoto mbalimbali.

Mkurugenzi wa Shirika la Room To Read- Tanzania, Bi. Joan Minja akizungumza kwenye maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Mtoto wa Kike yaliyoenda sambamba na uzinduzi wa Kitabu cha ‘She Creates Changes’ na video zinazoangazia mafanikio ya msichana aliyepitia changamoto mbalimbali.

Na Mwandishi Wetu, Dar

ALIYEKUWA Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Jokate Mwegelo amelipongeza Shirika la Room To Read- Tanzania kwa program zake zinazochochea wanafunzi nchini kusoma vitabu mbalimbali.

Alisema juhudi za shirika hilo kupitia program za hamasa za usomaji vitabu kwa kuanzisha maktaba na zile za mtandaoni, zimehamasisha wanafunzi kupenda kujisomea vitabu jambo ambalo linachochea hali ya ufaulu, na kuunga mkono juhudi za Serikali katika maboresho ya elimu nchini.

Kiongozi huyo mdau wa maendeleo ya elimu, ametoa kauli hiyo juzi jijini Dar es Salaam kwenye maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Mtoto wa Kike yaliyoenda sambamba na uzinduzi wa Kitabu cha ‘She Creates Changes’ na video zinazoangazia mafanikio ya msichana aliyepitia changamoto mbalimbali.

“Juhudi za Shirika la Room To Read- Tanzania za kuweka maktaba zaidi ya 1,500 na kuwasaidia maelfu ya wasichana katika mikoa ya Pwani, Tanga, Morogoro na Dar es Salaam zimeacha alama za kudumu katika jamii,” alisema, Bi. Jokate Mwegelo katika hotuba yake.

Aidha aliipongeza Serikali chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa jitihada mbalimbali za kuboresha elimu ikiwemo kutoa elimu bila malipo na ujenzi wa hosteli za wasichana jambo ambalo linapunguza vikwazo vya wanafunzi wa kike kwenye elimu.

“…Kupitia ushirikiano wa Shirika la Room To Read na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na Taasisi ya Elimu Tanzania, wamewezesha walimu kupata mafunzo ya ufundishaji unaozingatia jinsia na hivyo kuunda mazingira bora ya kujifunzia kwa wanafunzi wote,” alisisitiza kiongozi huyo aliyewahi pia kuwa Mkuu wa Wilaya za Kisarawe, Temeke pamoja na Korogwe,

Awali Mkurugenzi wa Shirika la Room To Read- Tanzania, Bi. Joan Minja aliishukuru serikali chini ya Uongozi wa Rais Samia kwa kuimarisha elimu kwa watoto wakiwamo wa kike kupitia mipango mbalimbali.

Alisema mipango mizuri ya serikali kama vile elimu hadi ngazi ya sekondari bila malipo, sera ya kuruhusu wasichana waliopata ujauzito kurudi shuleni na maboresho anuai ya sekta ya elimi inayofanya imechangia kuleta mabadiliko makubwa na kuwa ukombozi kwa wasichana na jamii kwa ujumla.

Bi. Joan, alibainisha kuwa kwa Tanzania, Room to Read imefanya kazi tangu mwaka 2012 katika mikoa ya Morogoro, Pwani, Tanga na Dar es Salaam ikilenga programu mbili za msingi ambazo ni usomaji na maktaba pamoja na elimu kwa msichana.

“Kwa Programu ya Elimu kwa Msichana, tunawasaidia wasichana kuanzia Darasa la 5 hadi Kidato cha 4 kukamilisha elimu yao ya sekondari wakiwa na stadi za maisha zinazohitajika ili kufanya uamuzi sahihi kufikia malengo binafsi na ya jamii zao,” alisema.

Bi. Joan, alisema nchini Tanzania Room to Read imefanikiwa kufikia wasichana takriban 16,000 kwa kuwajengea uwezo wa kupambana na changamoto mbalimbali vinazosababishwa na mila na desturi zikiwamo mimba na ndoa za utotoni, unyanyasaji wa kijinsia na umaskini.

 “…Aslimia 100 ya wasichana wanufaika wa mradi wameweza kuendelea na masomo kila mwaka, asilimia 90 ya wanufaika wa wameweza kufaulu mitihani ya taifa kidato cha pili na kidato cha nne, kupunguza mdondoko wa wanafunzi kutoka asilimia 18 mradi ulipoanza hadi asilimia 3 na asilimia 79 ya wasichana waliomaliza kidato cha nne wamejiunga na elimu ya juu…” alibainisha kiongozi huyo wa Room to Read nchini Tanzania.

No comments:

Post a Comment