LISHE NI MUHIMU KATIKA UTEKELEZAJI WA AFUA ZA AFYA KWA VIJANA BALEHE - DK HAONGA - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Monday 24 June 2024

LISHE NI MUHIMU KATIKA UTEKELEZAJI WA AFUA ZA AFYA KWA VIJANA BALEHE - DK HAONGA


Kaimu Mkurugenzi Huduma za Kinga kutoka Wizara ya Afya Dkt. Tumaini Haonga akizungumza katika Kikao na wawakilishi kutoka Nutritional International wakijadili afua za kuimarisha lishe kwa vijana balehe katika Ofisi za Idara ya Kinga zilizopo Itega Jijini Dodoma.


Na Elimu ya Afya kwa Umma

KAIMU Mkurugenzi wa Huduma za Kinga kutoka Wizara ya Afya Dkt. Tumaini Haonga amesema moja ya maeneo muhimu ambayo Serikali imejipambanua katika Sekta ya Afya ni eneo la lishe kwa vijana balehe.

Dkt. Haonga amebainisha hayo Juni 24, 2024 wakati akizungumza katika Kikao  baada ya kutembelewa na Wadau kutoka Nutrition International kwenye ukumbi wa Ofisi ya Idara ya Kinga uliopo Itega Jijini Dodoma kilicholenga kujadili afua mbalimbali za lishe kwa vijana balehe.

"Moja ya afua muhimu katika sekta ya afya ni afua ya lishe hususan kwa vijana balehe, hivyo kwenye eneo hili ni eneo muhimu sana, maana mtu hususan kijana balehe anapokuwa na lishe bora anakuwa na uwezo wa kufanya na kuchanganua mambo mfano kufanya vizuri darasani kwa umuhimu huo zinahitajika nguvu za  pamoja katika kuwekeza suala la lishe"amefafanua Dkt. Haonga.

Aidha, Dkt. Haonga amesema Serikali itaendelea kushirikiana na wadau kwani wana mchango mkubwa katika utekelezaji wa afua mbalimbali ikiwemo afua za lishe.

"Katika utekelezaji wa afua mbalimbali za afya Serikali imekuwa ikishirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo Nutrition Internation hivyo ninyi ni moja ya wadau muhimu na tutaendelea kushirikiana nanyi na katika eneo hili la lishe ni moja ya kipaumbele muhimu"amesema Dkt. Haonga.

Tumekuwa na mkutano wenye mafanikio makubwa kati ya Wizara ya Afya na wawakilishi kutoka shirika la Nutrition International leo tarehe 24 Juni 2024. Lengo la mkutano huu lilikuwa kuendeleza majadiliano ya afua za lishe kwa vijana balehe ili kuboresha hali ya lishe kwa vijana balehe nchini. Wizara ya Afya pia iliwakilishwa na mkurugenzi msaidizi wa huduma za lishe na wawakilishi kutoka Idara ya Huduma za Mama na Mtoto.

 Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Huduma za Lishe kwa Vijana balehe kutoka Shirika la Nutrition International(NI), Dkt. Anjali Bhardwaj amesema   wataendelea kufanya kazi kwa karibu na Wizara kutekeleza afua za lishe kwa vijana balehe.

"NI inaelekeza Mipango ya serikali ili kuhakikisha muendelezo hata baada ya miradi kufikia ukomo.

Mkurugenzi wa Nutritional International Dkt. George Mwita, ameahidi kuendeleza ushirikiano huo.

No comments:

Post a Comment