DK SAMIA ASHIRIKI MAADHIMISHO MIAKA 30 MAUAJI YA KIMBARI -RWANDA - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Sunday 7 April 2024

DK SAMIA ASHIRIKI MAADHIMISHO MIAKA 30 MAUAJI YA KIMBARI -RWANDA

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa pamoja na viongozi mbalimbali wakimshuhudia Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame akiwasha mwenge wakati wa kumbukumbu ya mauaji ya Kimbari Kigali nchini Rwanda tarehe 07 Aprili, 2024. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa pamoja na viongozi mbalimbali mara baada ya kuweka shada la maua kwenye eneo la Makaburi ya kumbukumbu ya mauaji ya Kimbari Kigali nchini Rwanda tarehe 07 Aprili, 2024. 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akielekea kwenye eneo la Makaburi kwa ajili ya kuweka shada la maua wakati wa Maadhimisho ya miaka 30 tangu kutokea mauaji ya Kimbari Kigali nchini Rwanda. Maadhimisho hayo ya miaka 30 yamefanyika katika Makumbusho ya Mauaji ya Kimbari, Kigali nchini Rwanda na kuhudhuriwa na viongozi kutoka nchi mbalimbali tarehe 07 Aprili, 2024. 


No comments:

Post a Comment