![]() |
| Kamishna Generali waMamlaka ya dawa za kulevya, Gerald Kusaya. |
Mwandishi Wetu
KOCHA wa Makipa wa Klabu ya Simba ya jijini Dar es Salaam Muharami Sultan (40) mkazi wa Kigamboni na wenzake wanane wanashikiliwa na Mamla ya Dawa za Kilevya nchini, kwa kukutwa na kilo 34.89 za herion.
Akizungumza na waandishi wa Habari ofisini kwake jijini Dar es Salaam, Kamishna Generali Gerald Kusaya wa Mamlaka ya kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya alisema mamlaka yake imefanikiwa kuwakamata watuhumia hao mahali tofauti nchini.
Alisema mbali na Sultani wengine ni, mmiliki wa kituo cha Cambiasso Sports Academy, Kambi Seif maarufu kama Alhaji Kambi (40) mkazi wa Oysterbay,Fundi Seremala, Said Matwiko (41) mkazi wa Kivule na mkulima, Maulid Mzungu maarufu kama Mbonde (54) mkazi wa Kamegele Kisemvule.
Wengine ni, mfanyabiasha John John maarufu kama Chipanda (40) mkazi wa Magore Kitunda, Rajabu Dhahabu (32) mkazi wa Tabata Segerea, mkulima Seleman Matola Said (24) ambaye ni mtoto wa dada yake Alhaji Kambi, Hussein Pazi (41) mkazi wa Kibugumo Kigamboni na Ramadhani Chalamila (27) mkazi wa Mzinga Kongowe.
Alisema bado upelelezi unaendelea kuwasaka watuhumia wengine na kwamba wakati wowote watuhumiwa watafikisha mahakamani.
Mbali na watuhumiwa tisa, mamlaka inawashikilia watuhumiwa wengine wawili kwa kukutwa na biskuti 50 zilizotengenezwa na Dawa za Kulevya aina ya bangi.
Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni, Abnasir Kombo mkazi wa Kaloleni Arusha akiwa na biskuti 50 zilizotengenezwa na bangi.
Mwingine ni,mtengenezaji wa biskuti Hassan Ismail (25) mkazi wa Arusha.
"Serikali haijalala bado tunaendelea na msako nchi nzima kwa wakae wakijua magereza yako wazi na wanaotarajia kutajirika na Dawa za Kulevya wasijisumbue tutawadaka"alisema Kamishna Kusaya.
Alisema watanzania wote washirikiane na mamlaka kufichua wanaojihusisha na Dawa za Kulevya nchini kuokoa maisha ya watanzania.


No comments:
Post a Comment