SHIMIWI WACHAGUANA MKOANI MOROGORO - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Sunday, 19 June 2022

SHIMIWI WACHAGUANA MKOANI MOROGORO

 

Mwenyekiti wa Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI), Daniel Mwalusamba akila kiapo baada ya kuchaguliwa tena na Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa shirikisho hilo kwa kura 70 kati ya 100 uliofanyika jana kwenye ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Mount Uluguru, mkoani Morogoro.


Mmoja wa wajumbe wa uchaguzi mkuu wa Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI), Mohamed Ally (wapili kulia) akisimamia zoezi la kuhesabu kura za wagombea wa nafasi ya ujumbe wa kamati ya utendaji katika uchaguzi uliofanyika jana kwenye ukumbi wa Hoteli ya Mount Uluguru, mkoani Morogoro.

Msimamizi wa uchaguzi mkuu wa Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI), Leonard Thadeo (aliyenyoosha kidole) wakati akizungumza na wajumbe waliokasimiwa madaraka na Baraza la Michezo la Taifa (BMT) kusimamia uchaguzi huo wakiwa wanazungumza mambo mbalimbali baada ya zoezi hilo kukamilika jana kwenye ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Mounti Uluguru, mkoani Morogoro.

Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI), wakifurahia jambo wakati wa mchakato wa upigaji kura uliofanyika jana kwenye ukumbi wa mikutano wa hoteli ya Mount Uluguru,, mkoani Morogoro.

No comments:

Post a Comment