KATIBU MKUU UJENZI ASISITIZA UBORA, UTEKELEZAJI WA MRADI - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Friday, 17 June 2022

KATIBU MKUU UJENZI ASISITIZA UBORA, UTEKELEZAJI WA MRADI

Mhandisi wa Miradi, kutoka Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS), mkoa wa Dodoma, Mhandisi Colman Gaston, akitoa taarifa ya maendeleo ya mradi wa barabara ya mzunguko wa nje ya jiji la Dodoma kwa katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi,(Sekta ya Ujenzi) Balozi. Aisha Amour, mara baada ya kukagua mradi huo.

KATIBU Mkuu wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi ( Sekta ya Ujenzi),  Balozi Mhandisi Aisha Amour, amewataka wakandarasi wanaotekeleza mradi wa ujenzi wa barabara ya mzunguko ya jiji la Dodoma na kiwanja cha ndege cha Msalato kuhakikisha wanazingatia viwango vya ubora katika utekelezaji wa miradi hiyo.

Akizungumza mara baada yakagua utekelezaji wa miradi hiyo jijini hapo, Balozi Aisha amesema kuwa kufanya hivyo kutawezeshamiradi hiyo kudumu kwa muda mrefu na kuweza kutumika kwa vizazi vya  sasa na vijavyo.

"Sisi kama Serikali tunataka kuona ubora wa kazi, miradi hii ikikamilika vizuri na kwa ubora itarahisisha huduma za usafiri na usafirishaji kwa wananchi wa Dodoma na mikoa jirani na hivyo kuleta maendeleokwa mtu mmoja mmoja na nchi kwa ujumla", amesema Balozi Aisha.

Aidha, Katibu Mkuu huyo amewataka makandarasi hao kuhakikisha kuwa wanatatua mapema changamoto zote zinazowakabili ili kuhakikisha miradi hiyo haikwami na inakamilika kwa wakati kama ilivyo kwenye mkataba.

Ameusisitiza Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) mkoani humo, kukagua na kufuatililia kwa karibu hatua kwa hatua utekelezaji wa miradi hiyo ili kuona kuwa thamani ya fedha inayotumika inaendana na mkataba.

Kwa upande wake, Kaimu Meneja wa TANROADS mkoa wa Dodoma, Mhandisi Salome Kabunda, amesema kuwa kwa sasa ujenzi wa mradi huu sehemu ya kwanza ya Nala- Veyula- Mtumba- Ihumwa Bandari Kavu ( Km 52.3) umefikia asilimia 8.5 na unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba 2024.

Kwa upande wa Kiwanja cha ndege cha Msalato, Mhandisi Kabunda amesema kuwa hadi sasa Mkandarasi amekwishamaliza ujenzi wa kambi  yake ya kuishi, karakana, boharipamojana mtambo wa kuzalisha kokoto na tofali.

Ameongeza kuwa ujenzi wa Kiwanja hiki unatarajiwa kujengwa kwa sehemu mbili ambapo sehemu ya kwanza itahusisha ujenzi wa miundombinu ambayo itajumuisha sehemu ya kurukia ndege, sehemu ya kupaki, njia ya ndege, maegesho ya magari, uzio, mageti pamoja na barabara za maingilio.

Mradi wa ujenzi wa Kiwanja cha ndege cha Msalato unajengwa na Mkandarasi Sinohydro Corporation Limited kwa kushirikiana na  M/s Beijing Sino - Aero Construction  Engineering  Co. Ltd na M/s China Jiangxi  International Economic  and Technical Cooperation na unatarajiwa kukamilika mwezi Aprili, 2025.

No comments:

Post a Comment