MHE. RAIS SAMIA ATUNUKU NISHANI NA SHAHADA KWA WAHITIMU WAPYA JWTZ MONDULI ARUSHA - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Monday 22 November 2021

MHE. RAIS SAMIA ATUNUKU NISHANI NA SHAHADA KWA WAHITIMU WAPYA JWTZ MONDULI ARUSHA

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akimvalisha bawa 2lt. Ibrahim Joseph Mwamboli kuashiria kuhitimu kozi ya Urubani kati ya Maafisa  wapya wanafunzi 56 wa JWTZ katika Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi Monduli (TMA) mkoani Arusha   leo tarehe 22 Novemba, 2021. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akifunga mafunzo kwa wahitimu wapya katika ngazi ya Shahada ya Sayansi ya Kijeshi katika masomo ya kiraia kwa Wahitimu 61 wa JWTZ katika Mahafali ya pili ya Chuo cha Uhasibu yaliyofanyika Monduli mkoani Arusha leo tarehe 22 Novemba 2021.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi, Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na wahitimu wapya katika ngazi ya Shahada ya Sayansi ya Kijeshi katika masomo ya kiraia katika Mahafali ya pili ya Chuo cha Uhasibu Monduli Arusha leo tarehe 22 Novemba 2021.

Wananchi na wageni wakifuatilia sherehe za kuwatunuku Kamisheni Maafisa wanafunzi  kundi la 02/18 wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) zilizofanyika kwenye Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi Monduli (Tanzania Millitary Academy - TMA) mkoani Arusha   leo tarehe 22 Novemba 2021.

Sherehe za kuwatunuku Kamisheni Maafisa wanafunzi  kundi la 02/18 wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) zilizofanyika kwenye Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi Monduli (Tanzania Millitary Academy - TMA) mkoani Arusha   leo tarehe 22 Novemba 2021.

Maafisa wapya wa JWTZ katika Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi Monduli mkoani Arusha leo tarehe 22 Novemba 2021.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akimvalisha bawa Slt. Asnat Rashid Akbar kuashiria kuhitimu  katika kozi ya Urubani kati ya Maafisa wapya wanafunzi 56 wa JWTZ katika Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi Monduli (Tanzania Military Academy-TMA) mkoani Arusha   leo tarehe 22 Novemba, 2021.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akitunuku Shahada ya Sayansi ya Kijeshi katika masomo ya kiraia kwa Wahitimu 61 wa JWTZ katika Mahafali ya pili ya Chuo cha Uhasibu yaliyofanyika TMA Monduli mkoani Arusha leo tarehe 22 Novemba, 2021.

No comments:

Post a Comment