TARI YATOA MAFUNZO YA AGRONOMIA YA KOROSHO KWA MAAFISA UGANI NA WAKULIMA KONGWA - THE HABARII
.com/img/a/
ASAS GROUP
.com/img/a/

Friday, 25 September 2020

demo-image

TARI YATOA MAFUNZO YA AGRONOMIA YA KOROSHO KWA MAAFISA UGANI NA WAKULIMA KONGWA

_MG_4993
Mtafiti  kutoka Tari- Naliendele Programu ya Zao la Korosho, Kasiga Ngiha, akitoa mafunzo ya jinsi ya kuandaa shamba, kulipima na upandaji wa zao la korosho kwa Maafisa Ugani na Wakulima wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa katika shamba la Shule ya Sekondari ya Mnyakongo.

_MG_4997
Mtafiti  kutoka Tari- Naliendele Programu ya Zao la Korosho, Kasiga Ngiha, akitoa mafunzo ya jinsi ya upimaji wa shamba kabla ya kupanda korosho.

_MG_5005
Afisa Kilimo kutoka Kata ya Songambele, Asha Malekela wa Wilaya ya Kongwa akipima shamba kwa kamba katika mafunzo hayo kwa vitendo. 


_MG_5009
Maafisa Ugani na Wakulima wakijifunza kwa vitendo namna ya upimaji wa shamba la korosho kabla ya kupanda.

_MG_5012
Mkulima Gasper Rupia kutoka Kijiji cha Ibwaga,  akijifunza namna ya kupima shamba wakati wa mafunzo kwa vitendo. Kulia ni Mkulima Raheli Esau kutoka kijiji hicho.


_MG_5016
Afisa Kilimo, Said Kajagale  kutoka Kata ya Ngomai akijifunza kunyoosha mstari kwa kuelekeza kwa mkono katika mafunzo hayo ya vitendo. 

_MG_5020
Afisa Kilimo kutoka Kata ya Mkoka, Marcelin Chingilile (kushoto) na wenzake wakiwa kwenye mafunzo hayo

_MG_5024
Afisa Kilimo kutoka Wilaya ya Kongwa, Elias Chilemue (kushoto) na wenzake, wakijifunza kutoka TARI namna ya kuweka alama wakati wa mafunzo kwa vitendo ya upimaji wa shamba la korosho.

_MG_5027
Afisa Kilimo kutoka Wilaya ya Kongwa, Dominica Swai (kushoto) akijifunza namna ya kuweka mambo wakati wa mafunzo kwa vitendo ya upimaji wa shamba la korosho.

_MG_5030
Mratibu wa Kitaifa wa Zao la Korosho kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo TARI Naliendele Mtwara, Dkt.Geradina Mzena (kulia), akielekeza namna ya kunyosha mstari kwa kamba katika mafunzo hayo. 

_MG_5042
Mkulima  Richard Sanyaji kutoka Kata ya Songambele ,  akishiriki mafunzo kwa vitendo kwa kuchimba mashimo katika shamba hilo la mfano la korosho la Shule ya Sekondari Mnyakongo.

_MG_5044
Mkulima Gasper Rupia kutoka Kijiji cha Ibwaga,  akijifunza namna ya kuchanganya udongo na samadi kabla ya kupanda korosho.

_MG_5056
Afisa Kilimo kutoka Kata ya Chitego, Michael Edward,  akishiriki mafunzo kwa vitendo kwa kuchimba mashimo katika shamba la mfano la korosho la Shule ya Sekondari Mnyakongo.

_MG_5066
Mtafiti wa Kilimo kutoka  Tari Naliendele, Selemani Libaburu,  akitoa mafunzo ya jinsi ya kupanda korosho katika  shamba la mfano la korosho la Shule ya Sekondari Mnyakongo.

Halotel+Mpango+Mzima

No comments:

Post a Comment

Contact Form

Name

Email *

Message *

Contact Form

Name

Email *

Message *