DANIEL TOROITICH ARAP MOI: WAKENYA WATOA HESHIMA ZA MWISHO KWA RAIS MSTAAFU - THE HABARII
.com/img/a/
ASAS GROUP
.com/img/a/

Saturday, 8 February 2020

demo-image

DANIEL TOROITICH ARAP MOI: WAKENYA WATOA HESHIMA ZA MWISHO KWA RAIS MSTAAFU

_110818238_a40198de-8070-4d0b-9ce7-321d5d56331f
Rais mstaafu Daniel Toroitich Moi

MWILI wa rais mstaafu wa Kenya Daniel Toroitich Arap Moi umewasili katika bunge kutoka chumba cha kuhifadhi maiti cha Lee Funeral jijini Nairobi mapema leo.

Wakenya kutoka matabaka mbalimbali tayari wameanza kuutazama mwili huo wa kiongozi huyo wa zamani .


habari-514254

Hatua hiyo inajiri baada ya rais Uhuru Kenyatta aliewasili kutoka nchini Marekani mapema leo kuwa mtu wa kwanza kuutazama mwili huo.


_110818472_040f0703-43e2-4493-b539-7074b616c9f5
Rais Uhuru Kenyatta na mkuu wa majeshi Meja jenarali samuel Mwathethe

Uhuru alipokewa na naibu wake wa rais William Ruto na mkuu wa majeshi Samson Mwathethe huku usalama ukiimarishwa.

Ruto aliwasili katika majengo ya bunge mwendo wa saa tatu na dakika 50 akiandamana na maafisa wa serikali.

_110818474_1f21084b-4a42-4a4b-b7b5-3bb88dda9fcf
Rais Uhuru Kenyatta na mkewe wakitoa heshima zao za mwisho kwa rais mstaafu Danile Moi

Kwa sasa viongozi mbalimbali wanautazama mwili huo.

Msafara wa gari lililokuwa likiusafirisha miwli huo kutoka chumba cha Lee ulipitia barabara ya alley Road na kuingia Kenyatta Avenue kabla ya kuingia katika barabara ya bunge ambapo gwaride la
kijeshi lilifanywa kutoa heshima.



84326626_3228455320516316_1617116239904112640_o
habari-51425452

Moi ambaye aliaga dunia siku ya Jumanne akiwa na umri wa miaka 95 atazikwa nyumbani kwake huko kabarak katika kaunti ya Nakuru tarehe 12 mwezi Februari.

_110818467_e1125281-440a-449f-863d-4dd6a2fb6928
Wakati rais Uhuru Kenyatta alipowasili katika majengo ya bunge kutoa heshima zake za mwisho kwa marehemu rais Mstaafu Daniel Moi

Serikali ilitangaza siku ya Jumanne tarehe 11 mwezi Februari kuwa siku kuu kwa raia kushiriki katika ibada ya mazishi ya mwili wa kiongozi huyo wa zamani.

Kwa sasa wananchi waliopanga milolongo mirefu wamepewa fursa kuutaza mwili huo .Shuguli ya kuutazama mwili huo itafanyika kwa siku tatu hadi lkufikia Jumatatu.


_110818242_769a35a8-a635-46f0-88c4-ebafd787c4c1
Wakenya waliojitokeza katika maeneo ya bunge la Kenya ili kutoa heshima zao za mwisho kwa rais mstaafu Daniel arap Moi
_110818688_8e49cb1c-224b-4973-a04d-10af0d223834
Wakenya wakizidi kumiminika ndani ya majengo ya bunge ili kutoa heshima kwa zao za mwisho kwa rais mstaafu Daniel Moi

Tangazo kutoka Ikulu lilisema kuwa mzee Moi, hata baada ya kuondoka madarakani aliendelea kulitumikia taifa la Kenya na Afrika kwa kuwafundisha viongozi wa Kenya na nje ya Kenya, akiendelea kushiriki kwenye maendeleo ya miradi mbalimbali na kazi za misaada akiihubiri amani, upendo na umoja barani Afrika na duniani.

Mzee Moi aliiongoza Kenya kuelekea kurudisha mfumo wa vyama vingi na katika vipindi vingine vingi vya changamoto; na kumalizika kwa mchakato wa kukabidhi madaraka kwa amani mwezi Desemba mwaka 2002, wakati huo mchakato ambao ulikuwa nadra kufanyika Afrika, ambao uliweka mfano barani afrika na nje ya bara tangu wakati huo.

''Hiba yake inaishi Kenya hata leo. Filosofia ya Nyayo kuhusu 'amani, upendo na umoja' ilikuwa wimbo wake kipindi chake kama kiongozi wa nchi na serikali''. Ilieleza taarifa ya Ikulu.

-BBC
Halotel+Mpango+Mzima

No comments:

Post a Comment

Contact Form

Name

Email *

Message *

Contact Form

Name

Email *

Message *