RC MAKONDA AFURAHISHWA NA KASI YA UJENZI WA MACHINJIO - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Monday 14 October 2019

RC MAKONDA AFURAHISHWA NA KASI YA UJENZI WA MACHINJIO


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akihamasisha mafundi Ujenzi wa Machinjio ya kisasa Vingunguti kwa kushiriki kazi hizo.



Ujenzi wa Machinjio ya kisasa ukiendelea Vingunguti jijini Dar es Salaam.


Ujenzi wa Machinjio ya kisasa ukiendelea Vingunguti jijini Dar es Salaam.


TANGU
Rais Dk. John Pombe Magufuli, alipotembelea ujenzi wa Machinjio ya Vingunguti hivi karibuni na kuangiza ujenzi huo uwe umekamilika ndani ya miezi mitatu ijayo, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ameendelea kusimamia ujenzi huo usiku na mchana.

Usimamizi huo unaonekana kuanzaa kuzaa matunda ya haraka jambo ambalo sasa anadai kufurahishwa na kasi ya ujenzi huo kiasi cha kumpa matumaini ya kukamilika ndani ya miezi mitatu iliyotolewa.

Akizungumzia ujenzi huo, Makonda amesema kuwa, katika jambo ambalo Watanzania walifanya kwa isahihi na kwamba hawatakuja kujuta kufuatia maendeleo yake, ni pamoja na kumchagua Rais Magufuli kuwa rais wa nchi hii.

Kwa maana hiyo uamuzi wa kufanya hivyo hakika wanatakiwa kutambua kuwa walichagua maendeleo ya ujenzi wa miundombuni sahihi kama, mabarabara,Hospitali,shule na sasa machinjio makubwa na ya kisasa kabisa ya vingunguti.

Kwa maana hiyo anawaomba watanzania waendelee kuunga mkono juhudi zake kwani yeye na viongozi wengine hawatachoka kumsaidia ili kufikia malengo bora aliyokusuhudia kuwafanyia watanzania wote kipindi chote cha uongozi wake.

No comments:

Post a Comment