RAIS UHURU KENYATTA AMALIZA ZIARA YAKE BINAFSI YA SIKU MBILI CHATO MKOANI GEITA NA KUREJEA NCHINI KWAKE - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Saturday 6 July 2019

RAIS UHURU KENYATTA AMALIZA ZIARA YAKE BINAFSI YA SIKU MBILI CHATO MKOANI GEITA NA KUREJEA NCHINI KWAKE

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na  mgeni wake Rais wa Kenya Mheshimiwa Uhuru Kenyatta ambaye aliambatana na ujumbe wake kutoka Kenya katika ziara yake binafsi ya siku mbili katika kijiji cha Mlimani Chato Mkoani Geita.

Rais wa Kenya Mheshimiwa Uhuru Kenyatta akiweka shada la maua katika moja ya makaburi ya Familia ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli yaliyopo katika kijiji cha Mlimani Chato wakati akiwa katika ziara yake binafsi ya siku mbili.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimsindikiza mgeni wake Rais wa Kenya Mheshimiwa Uhuru Kenyatta wakati wakipita kwenye Gadi ya Heshma iliyoandaliwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ katika uwanja wa Ndege wa Chato mkoani Geita.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na mgeni wake Rais wa Kenya Mheshimiwa Uhuru Kenyatta katika uwanja wa ndege wa Chato mara baada ya kumaliza ziara yake binafsi ya siku mbili Chato mkoani Geita.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha na  mgeni wake Rais wa Kenya Mheshimiwa Uhuru Kenyatta kabla ya kuanza mazungumzo yao Chato mkoani Geita.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimpungia mkono mgeni wake Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta wakati akipanda ndege kurejea nchini Kenya. PICHA NA IKULU.


No comments:

Post a Comment