SIKU YA HALI YA HEWA DUNIANI, WADAU WA TMA WAIFAGILIA...! - THE HABARII
.com/img/a/
ASAS GROUP
.com/img/a/

Saturday, 23 March 2019

demo-image

SIKU YA HALI YA HEWA DUNIANI, WADAU WA TMA WAIFAGILIA...!


DSC_0440
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Isack Kamwelwe (kushoto) akihutubia wadau wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) katika maadhimisho ya Siku ya Hali ya Hewa Duniani iliyoandaliwa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA).

DSC_0412
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC), Eng. Japhet Loisimaye akielezea namna taarifa zinazotolewa na TMA zinavyowasaidia wadau wa mamlaka hiyo kutekeleza majukumu yao, kwenye  hafla ya maadhimisho ya siku ya Hali ya Hewa Duniani iliyoandaliwa na TMA jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka za Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dk. Agnes Kijazi, Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA), Hamza Johari pamoja na Kaimu Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania, Elias Mwashiuya (kulia).

DSC_0389
Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA), Hamza Johari (katikati) akielezea jinsi taarifa zinazotolewa na TMA zinavyowasaidia wadau wa usafiri wa anga kutekeleza majukumu yao, kwenye  hafla ya maadhimisho ya siku ya Hali ya Hewa Duniani iliyoandaliwa na TMA jijini Dar es Salaam. Wengine ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka za Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dk. Agnes Kijazi (kushoto) na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC), Eng. Japhet Loisimaye (kulia).

DSC_0402
Kaimu Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania, Elias Mwashiuya akielezea namna wanavyonufaika na utabiri wa TMA kwenye hafla ya maadhimisho ya siku ya Hali ya Hewa Duniani iliyoandaliwa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA), Hamza Johari, na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC), Eng. Japhet Loisimaye wakiwa katika hafla hiyo.

DSC_0444
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka za Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dk. Agnes Kijazi (kushoto) akizungumza na wadau wa TMA katika maadhimisho ya siku ya Hali ya Hewa Duniani iliyoandaliwa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA). Kulia ni wadau wa TMA wakiwa kwenye maadhimisho hayo.
DSC_0460
Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya TMA, Dk. Buruhani Nyenzi (kushoto) akimpongeza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Isack Kamwelwe (katikati) mara baada ya kuwahutubia wadau wa Mamlaka za Hali ya Hewa Tanzania (TMA) kwenye maadhimisho hayo. Kulia ni Dk. Kijazi akifuatilia.
DSC_0377
 Wafanyakazi wa TMA wakiigiza igizo kuonesha umuhimu wa taarifa za utabiri kwenye maadhimisho ya Siku ya Hali ya Hewa Duniani iliyoandaliwa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA).
DSC_0365
Maadhimisho hayo yakiendelea.

DSC_0454
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Isack Kamwelwe (katikati) akitoa maelekezo kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka za Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dk. Agnes Kijazi (kulia) mara baada ya maadhimisho hayo. Kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya TMA, Dk. Buruhani Nyenzi akifuatilia.

DSC_0360
Wadau wa TMA wakifuatilia igizo kwenye maadhimisho ya Siku ya Hali ya Hewa Duniani iliyoandaliwa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA).
Halotel+Mpango+Mzima

No comments:

Post a Comment

Contact Form

Name

Email *

Message *

Contact Form

Name

Email *

Message *