TANROADS NA JICA WASAINI MKATABA UPANUZI BARABARA YA MWENGE-MOROCCO - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Thursday 28 February 2019

TANROADS NA JICA WASAINI MKATABA UPANUZI BARABARA YA MWENGE-MOROCCO

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Isack Kamwelwe akifafanua jambo katika hafla ya kusaini makubaliano ya ujenzi wa Barabara ya Morocco- Mwenge KM 4.3 kati ya Tanroads na Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA) jijini Dar es Salaam leo.

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Nchini (Tanroads), Eng. Patrick Mfugale (kushoto) na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA), Bw. Hayakazu Yoshida (kulia) wakisaini makubaliano ya ujenzi wa Barabara ya Morocco-Mwenge KM 4.3 jijini Dar es Salaam leo.

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Nchini (Tanroads), Eng. Patrick Mfugale (kushoto) na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA), Bw. Hayakazu Yoshida (kulia) wakibadilishana hati za mkataba mara baada ya kusaini makubaliano ya ujenzi wa Barabara ya Morocco-Mwenge KM 4.3 jijini Dar es Salaam leo.

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Nchini (Tanroads), Eng. Patrick Mfugale (kushoto) akitoa maelezo mafupi katika hafla ya kusaini makubaliano ya ujenzi wa Barabara ya Morocco-Mwenge KM 4.3 kati ya Tanroads na Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA) jijini Dar es Salaam leo.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, Mh. Hawa Mchafu Chakoma akifafanua jambo katika hafla ya kusaini makubaliano ya ujenzi wa Barabara ya Morocco-Mwenge KM 4.3 kati ya Tanroads na Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA) jijini Dar es Salaam leo.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Isack Kamwelwe (wa pili kulia) pamoja na viongozi wengine meza kuu wakifuatilia matukio anuai katika hafla ya kusaini makubaliano ya ujenzi wa Barabara ya Morocco-Mwenge KM 4.3 kati ya Tanroads na Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA) jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni Katibu Mkuu sekta ya Ujenzi Arch. Elius Mwakalinga.

Baadhi ya watendaji wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano pamoja na wawakilishi wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA) katika hafla ya kusaini makubaliano ya ujenzi wa Barabara ya Morocco-Mwenge KM 4.3.
Imeandaliwa na Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.


No comments:

Post a Comment