![]() |
| Sehemu ya madhimiso ya kilele cha Siku ya Wakulima nchini (Nane nane). |
Na Mwandishi Wetu, SIMIYU
BENKI ya NMB
imetoa mafunzo kwa zaidi ya Vyama Vya Msingi 1, 000 vya Ushirika wa
Wakulima
(AMCOS) ya kilimo na utunzaji fedha ndani ya Mwaka mmoja yenye lengo la
kuboresha
sekta ya kilimo nchini.
Akizungumza
na waandishi wa habari jana katika madhimiso ya kilele cha siku ya
wakulima
nchini (Nane nane) Mkoani Simiyu, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB -
Ineke
Bussemaker alisema benki yake imemaua kusaidia kuboresha sekta ya kilio
kutokana na
umuhimu wake katika kuchangia ukuaji wa uchumi wa nchi na pia
kuboresha
uchumi wa wakulima.
Alisema kuwa
mafunzo hayo ambayo bado yanaendelea sehemu mbali mbaloi nchini
yanatariwa
kuwafikia wakulima wengi zaidi kupitia vyama vya ushirika na hivyo
vitawezesha
kuboresha kilimo na kuleta mabadiliko ya kiuchumi katika ngazi ya jamii na
nchi kwa
ujumla.
Alisema kuwa
sekta ya kilimo ni uti wa mgongo wa uchumi wa nchi na kuajiri watanzania
zaidi ya
asilimia 70, hivyo inapaswa kuboreshwa ili kutoa mchangomkubwa katika
maendeleo ya
kiuchumi.
Bi.
Bussemaker alisisitiza kuwa unatakiwa ushirikiano wa wadau mbalimbali wa
mendeleo ili
kusaidia sekta ya kilimo kukua kwa haraka na kuleta tija kwa wakulima na
nchi kwa
ujumla na kuwa ikiachiwa serikali peke yake haitaweza kuleta mabadiriko hayo
kwa haraka.
Alisema kuwa
benki yake inaamini kuwa sekta ya kilimo inao uwezo mkubwa wa kuleta
mapinduzi ya
kweli katika uchumi endapo kilimo kitaboreshwa nchini na kwamba sekta
hiyo itakuwa
na mchango mkubwa katika kufikia malengo ya serikali ya uchumi wa
viwanda.
Bi.
Bussemaker alisema kuwa mbali na mafunzo hayo benki yake imekwisha tumia zaidi
ya shilingi
bilioni 100 katika kuboresha sekta ya kilimo nchini kwa kutoa mikopo
mbalimbali
pamoja na huduma zingine za kifedha kwa wakulima nchini.
“Ndani ya
miaka michache ijayo, tunatarajia kutumia kiasi cha shilingi bilioni 500 katika
sekta
kuwezesha shughuli za kilimo katika mnyororo mzima wa thamani, hivyo
nawaomba
wakulima kuto kukata tamaa na kilimo kwani benki yao ipo pamoja nao
katika
kuhakikisha inaleta mageuzi ya kilimo kwa manufaa na amendeleo ya wakulima
na nchi kwa
ujumla” alisema Bi. Bussemaker.
Bi.
Bussemaker aliwataka wakulima kutumia NMB Bank katika kuleta mageuzi chanya
katika
kilimo na kuinua uchumi wa Tanzania kufikia uchumi wa kati kwa kuzalisha
malighafi
zaidi ndani ya nchi ambazo zitatumika katika viwanda vilivyopo nchini kwa
kuwa mkulima
akilima zaidi viwanda vinapata malighafi zaidi.



No comments:
Post a Comment