Na Lusungu Helela-Dar es Salaam
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete
amesema Mfumo wa Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma (HRA)
hauna lengo la kumuondoa kazini ama kuwaonea watumishi wa umma hivyo hawana
sababu ya kuuhofia mfumo huo.
Mhe. Kikwete amebainisha hayo wakati wa
ufungaji wa mafunzo ya siku tatu kwa watumishi wa umma kutoka Taasisi ya Tiba
ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) Shirika la Masoko Kariakoo na Bodi ya
Sukari Tanzania yaliyofanyika MOI.
Amesema lengo la mfumo huo ni kuiwezesha kupima
utendaji wa watumishi wake kwa njia rahisi na kuongeza ufanisi wenye tija
kazini.
“Mfumo huu hauna lengo la kukomoa watu,
tunatakuwa na utumishi wa umma unaotimiza majukumu, utawezesha kupamga utumishi
wenye tija, huna sababu ya kuhofia” amesema Mhe: Kikwete
Amesema mifumo hiyo inakwenda kuonesha wapi kwenye
mapungufu ili paweze kuboreshwa
Aidha aliipongeza MOI kwa kutoa huduma bora kwa
Watanzania na kuitaka kuendelea na kasi hiyo kwa maslahi ya umma.
“MOI inaendelea kuwa bora hii yote ni juhudi zako
Profesa Makubi na timu yako, hongera sana, tunahitaji utumishi wenye tija”
amesema
Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Prof. Abel Makubi
akimkaribisha Naibu Waziri huyo alimpongeza kwa kuitembelea MOI mara kwa mara
na kwamba hatua hiyo inaongeza ari kwa watumishi kufanya kazi kwa umahiri.




No comments:
Post a Comment