RAIS MSTAAFU JK ATUNUKIWA TUZO KWENYE KONGAMANO LA UBORA WA ELIMU, AKUBALI ULEZI...! - THE HABARII

THE HABARII

HABARI | MATUKIO | MICHEZO.


ASAS GROUP

Habari Mpya


Tuesday, 28 November 2023

RAIS MSTAAFU JK ATUNUKIWA TUZO KWENYE KONGAMANO LA UBORA WA ELIMU, AKUBALI ULEZI...!

Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete (kushoto) ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Global Partnership for Education akipokea tuzo maalum kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mtandao wa Elimu Tanzania (TenMeT), Bi. Faraja Nyalandu tuzo hiyo iliyotolewa na taasisi hiyo kutambua mchango mkubwa wa kiongozi huyo katika sekta ya elimu imeenda sambamba kuridhia kuwa mlezi wa Mtandao wa TEN/MET kwa sasa.


Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Global Partnership for Education akizungumza na washiriki wa Kongamano la Tatu la Kimataifa la Ubora wa Elimu (IQEC) mara baada ya kukabidhiwa tuzo yake, na Mwenyekiti wa Bodi ya Mtandao wa Elimu Tanzania (TenMeT), Bi. Faraja Nyalandu (hayupo pichani).

Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete (kushoto) ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Global Partnership for Education akipokea tuzo maalum kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mtandao wa Elimu Tanzania (TenMeT), Bi. Faraja Nyalandu tuzo hiyo iliyotolewa na taasisi hiyo kutambua mchango mkubwa wa kiongozi huyo katika sekta ya elimu imeenda sambamba kuridhia kuwa mlezi wa Mtandao wa TEN/MET kwa sasa. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu (Elimu), Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Dkt. Charles Msonde akimpongeza kwa kupiga makofi

Mdau wa elimu, Richard Mabala akichangia jambo mara baada ya kuanza kwa mijadala inayoendelea kwenye Kongamano la Tatu la Kimataifa la Ubora wa Elimu (3rd International Quality Education Conference – IQEC), linalofanyika katika Ukumbi wa Marquee, Serena Hotel jijini Dar es Salaam.
.

Kushoto ni mmoja wa wadau wa elimu akipata maelezo ndani ya Banda la HakiElimu nje ya Kongamano la Tatu la Kimataifa la Ubora wa Elimu (3rd International Quality Education Conference – IQEC).

Mkurugenzi Mtendaji wa HakiElimu, Dk. John Kalage (Wa kwanza kulia) akiongoza moja ya mjadala kwenye Kongamano la Tatu la Kimataifa la Ubora wa Elimu (3rd International Quality Education Conference – IQEC), unaoendelea Ukumbi wa Marquee, Serena Hotel jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mtendaji wa HakiElimu, Dk. John Kalage akiongoza moja ya mjadala kwenye Kongamano la Tatu la Kimataifa la Ubora wa Elimu (3rd International Quality Education Conference – IQEC), unaoendelea Ukumbi wa Marquee, Serena Hotel jijini Dar es Salaam.

Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Global Partnership for Education na mgeni wa heshima katika Kongamano la Tatu la Kimataifa la Ubora wa Elimu (IQEC), akitembelea mabanda mbalimbali ya wanachama wa Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET) wanaoshiriki katika Kongamano la Tatu la Kimataifa la Ubora wa Elimu (IQEC), linalofanyika katika Ukumbi wa Marquee, Serena Hotel jijini Dar es Salaam.


No comments:

Post a Comment