MBUNGE MATTEMBE AUNGA MKONO JITIHADA ZA RAIS DKT.SAMIA AZINDUA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI MKOA WA SINGIDA - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Thursday 5 October 2023

MBUNGE MATTEMBE AUNGA MKONO JITIHADA ZA RAIS DKT.SAMIA AZINDUA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI MKOA WA SINGIDA

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Singida Aysharose Mattembe akizungumza na wajasiriamali wakati akizindua mafunzo ya ujasiriamali Wilaya ya Mkalama mkoani hapa Oktoba 3, 2023ambayo yatafanyika katika wilaya zote. 

Na Dotto Mwaibale, Singida

MBUNGE wa Viti Maalum Mkoa wa Singida Aysharose Mattembe ameunga mkono jitihada za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuhakikisha wananchi wanajikomboa kiuchumi kwa kuzindua Mafunzo ya Ujasiriamali  Wilaya ya Mkalama mkoani Singida, mafunzo yenye kaulimbiu isemayo "SINGIDA YA UJASIRIAMALI NA SAMIA INAWEZEKANA"

Akizungumza wakati akizindua mfunzo hayo Mattembe alisema yamelenga  kuwawezesha wajasiriamali kujiamini na kuweza kutoka hatua moja kwenda nyingine kiuchumi.

"Mafunzo haya ambayo yatatolewa na wawezeshaji wabobezi ni muhimu sana kwa wananchi wetu na wajasiriamali kwani yanakwenda kuchochea uukuaji wa uchumi wao na kujikwamua kiuchumi," alisema Mbunge Mattembe.

Mafunzo hayo ambayo yatafanyika katika wilaya zote za Mkoa wa Singida yatahusisha usindikaji nafaka, matunda, ufugaji bora wa kuku, kilimo, pamoja na usimamizi wa fedha yameandaliwa na ofisi ya mbunge na yanatarajiwa kumalizika   November 10, 2023.

Aidha, Mattembe amewaomba wananchi kujitokeza kwa wingi kupata mafunzo hayo na washiriki wayazingatie kikamilifu na kuwa mabalozi wazuri kwa wengine ili tija iweze kupatikana maana ni mkombozi kwao na jamii kwa ujumla.

Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo walimshukuru Mbunge Mattembe kwa kuwajali wananchi na wajasiriamali kwa kuwapelekea mafunzo hayo yenye lengo la kuwakomboa kiuchumi na kuacha kuwa tegemezi.

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Singida Aysharose Mattembe akionesha namna  ya kupika wakati akizindua mafunzo hayo.
Mbunge Mattembe akiwa na Wajasiriamali wakati wa uzinduzi wa mafunzo hayo.
Mbunge Mattembe akionesha furaha yake wakati wa uzinduzi wa mafunzo hayo.

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Singida Aysharose Mattembe (wa pili kutoka kushoto waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo hayo wa Wilaya ya Mkalama.

 

No comments:

Post a Comment