MSAFARA WA BAISKELI WA TWENDE BUTIAMA WAWASILI JIJINI DODOMA - THE HABARII

THE HABARII

HABARI | MATUKIO | MICHEZO.


ASAS GROUP

Habari Mpya


Saturday, 9 April 2022

MSAFARA WA BAISKELI WA TWENDE BUTIAMA WAWASILI JIJINI DODOMA

 

Msafara wa Baiskeli wa Twende Butiama ukiwasili katika Ofisi za Wizara ya Maliasili na Utalii zilizopo mji wa Serikali, Mtumba Jijini Dodoma. Msafara huo wa waendesha baiskeli hao unaelekea Butiama katika kuadhimisha miaka 100 ya Hayati Julius Kambarage Nyerere.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Bw. Juma Mkomi akizungumza na Mkuu wa Msafara wa Baiskeli wa Twende Butiama Bw. Gabriel Landa wakati msafara huo ulipowasili katika Ofisi za Wizara hiyo zilizopo mji wa Serikali, Mtumba Jijini Dodoma ukielekea Butiama, Mkoani Mara katika kuadhimisha miaka 100 ya hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Mkuu wa Msafara wa Baiskeli wa Twende Butiama Bw. Gabriel Landa akielezea lengo la msafara huo ulioanzia Msasani nyumbani kwa mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam mpaka Butiama  katika kuadhimisha  miaka 100 ya Hayati Julius Kambarage Nyerere.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Bw. Juma Mkomi akitia saini ikiwa ni ishara ya waendesha baiskeli hao kufika Jijini Dodoma.

No comments:

Post a Comment