WAZIRI wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Elias Kuandikwa amefariki dunia jijini Dar es Salaam. Taarifa zilizotufikia zinaeleza kuwa Mhe. Elias Kuandikwa amefariki dunia jijini Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu. Elias John Kwandikwa ni mwanasiasa Mtanzania na mwanachama wa Chama cha Mapinduzi, CCM. Alichaguliwa kuwa mbunge wa Jimbo la Ushetu mwaka 2015 – 2020 ambapo umauti umempata; Kiongozi huyo aliyezaliwa Julai Mosi, 1966 ambaye ameshika nafasi mbalimbali serikalini hadi alipoteuliwa kuwa Waziri wa Ulinzi.
Habari kubwa Magazetini Kenya leo October 22, 2024
-
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania October 22,
2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na
za nyuma Magazetini...
59 minutes ago
No comments:
Post a Comment