KONGAMANO LA 'WOMAN OF INFLUENCE' LAJADILI MADHARA YA COVID 19 KWA WAJASILIAMALI AKINAMAMA - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Sunday 15 November 2020

KONGAMANO LA 'WOMAN OF INFLUENCE' LAJADILI MADHARA YA COVID 19 KWA WAJASILIAMALI AKINAMAMA

 

Mkurugenzi na Mwanzilishi wa Kampuni ya ZARA Tours, Bi. Zainab Ansell akizungumza kwenye 'Kongamano la Woman of Influence, I'm Possible'  jana kwenye Hotel ya Serena Dar es Salaam. Kongamano hilo pamoja na mambo mengine lilijadili namna wajasiriamali wanawake walivyo kabiliana na changa moto za janga la corona kwenye biashara zao.


Mkurugenzi wa Bang! Magazine, Bi. Emelda Mwamanga akizungumza na wanahabari (hawapo pichani) kwenye Kongamano la 'Woman of Influence, I'm Possible'  jana kwenye Hotel ya Serena Dar es Salaam. Kongamano hilo pamoja na mambo mengine lilijadili namna wajasiriamali wanawake walivyo kabiliana na changa moto za janga la corona kwenye biashara zao.


Mjasiliamali Bi. Leina Lemomo (kulia) akizungumza kwenye 'Kongamano la Woman of Influence, I'm Possible'  jana kwenye Hotel ya Serena Dar es Salaam. Katikati ni Mkurugenzi na Mwanzilishi wa Kampuni ya ZARA Tours, Bi. Zainab Ansell pamoja na Mwanzilishi wa Safe Space Group Araika Mkulo wakiwa katika mjadala kwenye kongamano hilo.


Mjasiliamali Bi. Leina Lemomo akizungumza kwenye 'Kongamano la Woman of Influence, I'm Possible'  jana kwenye Hotel ya Serena Dar es Salaam. Kongamano hilo pamoja na mambo mengine lilijadili namna wajasiriamali wanawake walivyo kabiliana na changa moto za janga la corona kwenye biashara zao.


Mmoja wa washiriki kwenye Kongamano la Woman of Influence, I'm Possible'  akijadili jambo katika kongamano hilo lililofanyika jana kwenye Hotel ya Serena jijini Dar es Salaam. 


Akinamama wajasiliamali waliofanikiwa, kutoka kulia ni Bi. Leina Lemomo, Mkurugenzi na Mwanzilishi wa Kampuni ya ZARA Tours, Bi. Zainab Ansell, Mwanzilishi wa Safe Space Group Araika Mkulo pamoja na Mkurugenzi wa Kampuni ya AKM Gliters Co LTD, Elizabeth Swai wakiwa katika mjadala kwenye Kongamano la Woman of Influence, I'm Possible'  jana kwenye Hotel ya Serena Dar es Salaam. 


Sehemu ya akinamama wajasiliamali na wageni mbalimbali wakifuatilia mijadala kwenye Kongamano la Woman of Influence, I'm Possible'  jana kwenye Hotel ya Serena Dar es Salaam. 

Na Joachim Mushi, Dar

AKINAMAMA Wajasiriamali mbalimbali wamekutana katika kongamano la 'Woman of Influence, I'm Possible' kujadili changamoto za ugonjwa wa Covid 19 nchini kwenye shughuli zao na kujadiliana namna ya kujikwamua na changamoto hizo. Kongamano hilo lililoratibiwa na Mkurugenzi wa The East Africa Bang! Magazine, Bi. Emelda Mwamanga limefanyika jana kwenye Hotel ya Serena jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na wanawake wajasiliamali na wageni mbalimbali ambapo mijadala na mada anuai ziliwasilishwa kuwajengea uwezo akinamama hao.

Akizungumza na wanahabari katika kongamano hilo, Bi. Emelda Mwamanga alisema lengo la kongamano hilo ni kuwakutanisha akinamama na kujadili changamoto zilizojitokeza, kushirikishana namna ya kukabiliana nazo na kuwajengea uwezo jamii hiyo kuweza kufanya vizuri zaidi kwenye shughuli zao kwa mwaka ujao wa 2021. Alisema sehemu kubwa ya biashara zikiwemo za kinamama ziliathirika kiasi kikubwa na ujio wa janga la corona, hivyo kuna kila sababu ya kuyajengea uwezo makundi mbalimbali wakiwemo akinamama wajasiriamali kuweza kukabiliana na janga hilo.

Alisema Bang Magazine wamekuwa chachu ya kutamani maendeleo ya akinamama ndio maana wamekuwa wakiwakutanisha kila mwaka tangu 2004, kusudi kubwa ikiwa ni kumjengea uwezo mwanamke kwa kuwakutanisha na wenzao waliofanikiwa zaidi ili waweze kuwasaidia wenzao kujikwamua zaidi kimafanikio.

Naye Mkurugenzi na Mwanzilishi wa Kampuni ya ZARA Tours, Bi. Zainab Ansell akizungumza kwenye Kongamano hilo, alisema wao kama wajasiriamali wanawake waliopo katika sekta ya utalii wamejipanga kuhamasisha utalii wa ndani ili kuziba pengo la upungufu wa watalii kutoka nje lililotokana na janga la corona.

"...Sisi toka sekta ya utalii tumeanza kuhamasisha utalii wa ndani kwa kuhamasisha jamii kuanza kutembelea sehemu zetu mbalimbali za vivutio vya utalii, tayari tumefanya hivyo hapo nyumba na sasa tunaandaa mapumziko ya mwezi Desemba, Siku Kuu ya Krismas wengine waweze kutembelea mbuga zetu anuai na hata kupanda Mlima wa Kilimanjaro," Bi. Zainab Ansell.

Alisema Tanzania ina sehemu nzuri na za kujivunia za utalii hivyo Watanzania wanatakiwa kuelimishwa na kuhamasishwa kuzitembelea; "Ukiangalia hata tozo za kutembelea mbuga zetu kwa Watanzania zipo chini sana ukilinganisha na za wageni kutoka nje ya nchi...kinachotakiwa ni kuelielimishwa na kuhamasishwa wao kutembelea rasilimali hizo za taifa," alisema. Aliongeza kuwa kampuni ya ZARA ina tozo maalum kwa Watanzania watakapenda kutembelea sehemu mbalimbali za vivutio vya utalii ikiwa ni kuchochea utalii wa ndani kwa jamii ya Watanzania.

Kwa upande wake, Mjasiliamali toka sekta ya utalii, Bi. Leina Lemomo amesema wameanzisha ushawishi wa tozo maalum za kiafrika (African rates) maeneo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuchochea utalii wa ndani. Amesema ndoto zao ni kuona kunakuwa na tozo maalum kwa Waafrika wanapotembelea nchi na maeneo mbalimbali ya bara la Afrika.

"Ndoto yetu ni kuona kwamba kunakuwa na tozo maalum kwa ajili ya waafrika tunapotembelea sehemu mbalimbali ndani ya Bara la Afrika, tunataka ukisafiri kiutalii hata kwenye ndege kuwepo na punguzo la malipo maalum kwa waafrika, vivyo hivyo kwenye hoteli mbalimbali barani Afrika...hii inawezekana na inaweza pia kuchochea utalii wa ndani kwa Waafrika. Ukienda mabara mengine tozo kama hizo zipo kwa raia wao na sisi hili kuna haja ya kulipigia debe sote kwa pamoja," alisema Bi. Lemomo.       


Mjasiliamali Bi. Leina Lemomo akizungumza na wanahabari (hawapo pichani) kwenye 'Kongamano la Woman of Influence, I'm Possible'.

Sehemu ya akinamama wajasiliamali na wageni mbalimbali wakifuatilia mijadala kwenye Kongamano la Woman of Influence, I'm Possible'  jana kwenye Hotel ya Serena Dar es Salaam. 

Sehemu ya akinamama wajasiliamali na wageni mbalimbali wakifuatilia mijadala kwenye Kongamano la Woman of Influence, I'm Possible'  jana kwenye Hotel ya Serena Dar es Salaam. 


Sehemu ya maonesho ya bidhaa mbalimbali yakiendelea katika kongamano hilo.

      

Sehemu ya maonesho ya bidhaa mbalimbali yakiendelea katika kongamano hilo.


Sehemu ya washiriki wakiwa katika banda la Bang! Magazine kwenye kongamano hilo.


Sehemu ya maonesho ya bidhaa mbalimbali yakiendelea katika kongamano hilo.



No comments:

Post a Comment