MAJALIWA ASHIRIKI MAZISHI YA WAZIRI KIONGOZI MSTAAFU WA ZANZIBAR - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Sunday, 29 March 2020

MAJALIWA ASHIRIKI MAZISHI YA WAZIRI KIONGOZI MSTAAFU WA ZANZIBAR

Rais wa Zanzibar, Dkt. Ali  Mohamed Shein akizungumza na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  katika mazishi ya Waziri Kiongozi  Mstaafu wa Zanzibar, Brigedia Jenerali Mstaafu, Ramadhani Haji Faki yaliyofanyika  Mkwajuni  Zanzibara Machi 29, 2020. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiweka udongo kwenye kaburi la Waziri Kiongozi wa Zanzibar Mstaafu, Brigedia Jenerali Mstaafu, Ramadhani Haji Faki yaliyofanyika  Mkwajuni  Zanzibar,  Machi 29, 2020. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Ali Mohamed Shein leo amongoza waombolezaji katika mazishi ya Waziri Kiongozi Mstaafu wa Zanzibar, Brigedia Jenerali Mstaafu, Ramadhani Haji Faki yaliyofanyika Mkwajuni  Zanzibar. 

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ambaye  amemwakilisha Rais Dkt. John Pombe Magufuli  katika mazishi hayo,  alipata fursa ya kutoa salamu za pole za Rais kwa wanafamilia na ndugu wa marehemu  baada ya mazishi .

Akitoa salamu za Serikali ya  Mapinduzi ya Zanzibar, Waziri wa Nchi , Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais  wa Zanzibar, Mohammed Abood amemuelezea marehemu kuwa ni kiongozi aliyekuwa mstari wa mbele kutetea haki na kusimamia maendeleo katika nchi yetu.

“Aliweka mbele maslahi ya taifa na kuweka mbali maslahi yake binafisi ndiyo maana alishiriki katika vita kati ya Tanzania na Uganda vilivyomundoa madarakani Nduli Iddi Amini.”

Marehemu alizaliwa mwaka 1930 katika kijiji cha Mkwajuni, Kaskazini Unguja na mwaka 1983 hadi 1984 alikuwa ni Waziri Kiongozi wa Zanzibar.

Wakati huo huo,  Waziri Mkuu leo ametoa pole kwa familia ya Waziri Mkuu  wa  zamani wa Tanzania, Hayati Edward Moringe Sokoine ambayo imeondokewa na  Lazaro Edward Sokoine,   aliyefariki Machi 28,2020 katika hospitali ya  taifa Muhimbili alikokuwa akitibiwa.

Kwa mujibu wa msemaji wa familia  Balozi Joseph Sokoine ambaye Pia ni Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais, kesho kutakuwa na misa ya kumuombea marehemu kwenye kanisa katoliki Parokia ya Mtakatifu Petro, Oysterbay jijini Dar es salaam. 

Amesema mazishi yanatarajiwa kufanyika katika kijiji cha Embwiki Monduli Juu  keshokutwa..

No comments:

Post a Comment