NMB YAWASAIDIA WAKANDARASI WAZAWA - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Monday 3 February 2020

NMB YAWASAIDIA WAKANDARASI WAZAWA

 Afisa Mkuu wa Wateja Bianfsi, Wafanyabiashara Wadogo na wa Kati – Filbert Mponzi akiteta jambo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano – Mhandisi Elius Mwakalinga kwenye hafla hiyo.


Kaimu Afisa Mkuu wa Wateja Wakubwa na Biashara ya Serikali – Aziz Chacha akiongea kwenye Hafla iliyowakutanisha Benki ya NMB na Wakandarasi wa Kanda ya Ziwa jijini Mwanza. Pembeni yake ni Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi, Wafanyabiashara Wadogo na wa Kati – Filbert Mponzi.

 Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano – Mhandisi Elius Mwakalinga akitoa maelezo ya Serikali kwenye mdahalo kati ya NMB na Wakandarasi kutoka Kanda ya Ziwa. 

BENKI  ya  NMB  mwaka jana  imetoa  zaidi  ya  dhamana  500  kwa  wakandarasi wazawa  ili  kuwawezesha  kugharimia  miradi  mbalimbali  ya  ujenzi  nchini. Mkakati  huo  ulifikiwa  kufuatia  kilio  cha  muda  mrefu  cha  wakandarasi  kushindwa kushiriki  katika  ujenzi  wa miradi  mbalimbali  kutokana  na  ukata  wa  fedha  na ushindani  toka  kwa  makampuni  ya  nje. 
Akiongea  wakati  wa  kongamano  lililohudhuriwa  na  zaidi  ya  wanadarasi  300 kutoka  Kanda  ya  Ziwa  mwishoni  mwa  wiki, Afisa Mkuu  wa  Wateja  Binafsi, Wafanyabiashara  Wadogo  na  wa Kati wa NMB Filibert  Mponzi alisema zoezi hilo litakua endelevu.

Alisema  mbali  na  kusaidia  kuwanyanyua  wakandarasi  wadogo  kimtaji,  pia  Benki hiyo  imeitikia  wito  wa  Rais  John  Magufuli  alioutoa juu  ya  taasisi  mbalimbali  za kibenki  kuwakopesha  wakandarasi  kwa  masharti  nafuu. “Kama  benki  ya  biashara  na  kama  mbia  wa  serikali  tumeshiriki  kikamilifu kuwasaidia  wakandarasi  kimtaji  na  pia  kuitikia  wito  wa  Rais  Magufuli  kuhakikisha kada  hiyo  inashiriki  kikamilifu  katika  ujenzi  wa  uchumi,”  alisema  Mponzi.

Mkakati  wa kutoa  dhamana  kwa  wakandarasi  umesaidia  sana  kuwawezesha kupata  kazi  za  uhakika  za  ujenzi  na  kwa  mujibu  wa  Mponzi  benki  inatoa  dhamana ya  asilimia  50  ya  thamani  ya  mradi  husika. Mbali  na  kutoa  dhamana  ya  mikopo  NMB  pia  itaanza  kutoa  huduma  ya  bima  kwa waka ndarasi  hao  kuwawezesha  kushiriki  kwa  ufanisi  zaidi  kwenye  miradi mbalimbali  kwa  riba nafuu. 

Hata  hivyo,  alisema wakati  benki  ikibuni  njia  mbalimbali  za  kuwasaidia wakandarasi  wadogo  na  wazawa  kuna  umuhimu  mkubwa  kwao  kuwa  waaminifu katika  urejeshaji  wa  mi kopo  na  kuheshimu  masharti  ya  dhamana  ili  kuepuka kulipa  riba  kubwa  kama  adhabu  baada  ya  mikataba  kukiukwa.

Katika  kongamano  hilo  lililohudhuriwa  pia  na  Katibu  Mkuu  wa  Wizara  ya  Ujenzi, Uchukuzi  na  Mawasiliano    Eliud  Mwakalinga  wakandarasi  walijadili  chan gamoto mbalimbali  na  kushauri  mikakati  mbalimbali  ya  kupambana  nazo.

 Akizungumza  nao,  Katibu  Mkuu  Mwakalinga  mbali  na  kuishukuru  NMB  kwa ubunifu  na  huduma  za  mikopo  na  dhamana  kwa  wakandarasi  wazawa  alisema kazi  za  ujenzi  zinahitaji  uaminifu  mkubwa  na  kuzi ngatia  ubora. Alisema  tafiti  mbalimbali  zinaonesha  wakandarasi  wazawa  hasa  wadogo wamekuwa  wakishindwa  kupewa  kazi  kubwa  kwa  zababu  kadhaa  zikiwamo  wengi kushindwa  kuajiri  wahandisi  waliobobea  na  wenye  weledi  usiotiliwa  shaka.

 “Tumefanya  utafiti  na  kugundu a  kuna  shida  kubwa  kwa  wakandarasi  wengi wadogo  kushindwa  kukaa  na  wahandisi  waliobobea  kwa  kukwepa  kuwalipa mishahara  wanayostahili  na  kuishia  kuajiri wahandisi  wanafunzi  na  hata  mafundi mchundo  tu,”  alisema.

Mhandisi Mwakalinga  alidokeza  mbinu  kadhaa  za kuwawezesha  wakandarasi wadogo  ikiwa  ni  pamoja  na  kuhakikisha  wanashindana  katika  kujenga  miradi mikubwa  inayoshikiriwa  na  makampuni  mengi  ya  nje. 

Kwa  upande  wake,  Mwenyekiti  wa  Chama  cha  Wakandarasi  Mkoani  Mwanza Mhandisi  Oscar  Munishi  aliwataka  wakandarasi  wazawa  kujitathmini  juu  ya uadilifu  wao  kazini  na  kwamba  kuna  mapungufu  kadhaa  yanayohitaji  kufanyiwa kazi  miongoni  mwao. Aliyashukuru  mabenki  yaliyojitokeza  kuwadhamini  kwa  mikopo  ya  riba  nafuu  na akaishukuru  NMB  kwa  kukutana  nao  na  kujadili  nao  namna ya  kuboresha  utendaji kazi  na  kushindana  kikamilifu sokoni. 
#NMBKaribuYako

No comments:

Post a Comment