WATU 20 wafariki
dunia mjini Moshi walipokuwa wakikusanyika katika viwanja vya Majengo
kuhudhuria Ibada iliyoongozwa na Mtume Boniface Mwamposa.
Watu hao wamefariki dunia baada ya
kukanyagwa na wenzao wakati wakitoka katika lango moja waliloelekezwa kupita
ili kukanyaga mafuta ya upako.
Katika tukio hili watu 16
wamejeruhiwa.
Kiongozi wa kanisa la Inuka Uangaze,
anayejitambulisha kama nabii na mtume Boniface Mwamposa , hii leo amelazimika
kusitisha ibada kwa ajili ya kuitikia wito wa Polisi mkoani Kilimanjaro,
Tanzania kulikotokea vifo vya waamini wake.
Mwamposa ambaye huendesha ibada zake
katika eneo la Tanganyika Packers, leo Jumapili Februari 2, Nabii huyo
amelazimika kufupisha ibada ya kwanza na kuanza safari ya kuelekea Moshi
alikoitwa na polisi.
Ibada huwa inaisha majira ya saa
saba lakini leo imeisha saa nne na nusu asubuhi.
Gazeti la Mwananchi limeandika kuwa
jana katika kongamano lake la kukanyaga mafuta ya upako mkoani Kilimanjaro,
watu 20 walipoteza maisha wakisukumana kukanyaga mafuta hayo.
Wakati hayo yakiendelea, waumini wa
nabii huyo wamemkingia kifua na kueleza suala la watu kukanyagana kwenye
mikutano mikubwa ni kawaida.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, John Pombe Magufuli ametuma salamu za rambirambi kwa familia za watu
20 waliopoteza maisha wakati wakitoka katika Ibada huko Moshi Mkoani
Kilimanjaro.
Magufuli ameeleza kusikitishwa na
idadi kubwa ya vifo vya Watanzania waliopoteza maisha katika matukio hayo na
amewaombea Marehemu wote wapumzike mahali pema peponi na majeruhi wote wapone
haraka na kurejea katika majukumu yao.
Aidha amemtaka mkuu wa mkoa wa
Kilimanjaro bi. Anna Mghwira kufikisha salamu zake za pole kwa familia, ndugu,
jamaa, marafiki na wote walioguswa na vifo hivyo.
Rais Magufuli ametoa wito kwa
Watanzania wote kuchukua tahadhali katika matukio yote yenye viashiria vya
hatari ikiwemo mikusanyiko mikubwa ya watu na amevitaka Vyombo vya Ulinzi na
Usalama kuhakikisha vinasimamia ipasavyo tahadhali za kiusalama.
-BBC
No comments:
Post a Comment