![]() |
Mafundi wakiendelea na
kazi ya ujenzi wa barabara ya Mzunguko wa Nje (Dodoma City Outer Dual
Carriageway Ring Road) unaoendelea jijini Dodoma
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Balozi, Mhandisi, Aisha Amour amemwagiza
mkandarasi anayejenga barabara ya mzungumzo jijini Dodoma kufanya kazi kwa
mujibu wa mkataba, kutekeleza maagizo anayopewa na viongozi wakati wa ukaguzi
wa miradi.
Alitoa maagizo hayo leo jijini Dodoma wakati akikagua mradi wa ujenzi
huo kwa kiwango cha lami wenye urefu wa km 112.3 sehemu ya Barabara ya Ihumwa
Dry Port- Matumbulu - Nala yenye urefu wa km 60.
Pamoja na mambo mengine, Balozi Aisha alimtaka
Mkandarasi huyo kuhakikisha anazingatia
ubora wa kila tabaka kabla ya kuendelea na tabaka lingine, kupima mali ghafi za
ujenzi, kuhakikisha ubora kabla ya kuzitumia ili kuzuia barabara hiyo
kuharibika kabla ya wakati.
“Hakikisheni mnatumia maabara vema na mkandarasi
ahakikishe vifaa vyote vya maabara vinakuwa eneo la ujenzi kipindi chote cha
utekelezaji wa mradi” alisema Balozi Aisha.
Pia, aliwataka kuhakikisha wanapambanua
mapungufu hayo na kuweka mkakati wa kuyafanyia kazi kwa wakati ili kuleta matokeo
chanya.
Aidha, amewataka kufanya kazi kwa kizingatia
misingi, kanuni na sheria za nchi ikiwa ni pamoja na kujiepusha na vitendo vya
rushwa maeneo ya kazi.
“Hakikisheni wafanyakazi hawajiingizi katika
vitendo vya rushwa kwa kupunguza mianya ya rushwa nyakati zote wakati mradi
unatelelezwa” alisisitiza Balozi Aisha.
Mradi wa mzunguko wa nje wa Jiji la Dodoma wenye
urefu wa km 112. umegawanywa katika sehemu mbili za utekelezaji ukijumuisha
Sehemu ya kwanza ya Nala - Nyeyula - Mtumba -
Ihumwa Dry Port (km 52.3) ambapo ujenzi wake umefikia zaidi ya asilimia 76 na
Sehemu ya pili ya Ihumwa Dry Port- Matumbulu -
Nala (km 60) ambapo ujenzi wake umefikia zaidi ya asilimia 60.




No comments:
Post a Comment