Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) MNEC
Teresia Mtewele akimuombea kura mgombea ubunge jimbo la Kalenga Jackson
Kiswaga ili aweze kushinda kwa kisindo katika uchaguzi wa mwaka
huu.
Mgombea ubunge wa jimbo la Kalenga kupitia chama cha mapinduzi Jackson
Kiswaga akieleza kwanini wananchi wa jimbo la Kalenga wanapaswa kumpigia
kura nyingi ili awe mbunge wao kwa maendeleo ya jimbo hilo.
Mjumbe wa halmashauri kuu ya taifa ya chama cha mapinduzi (CCM) MNEC
Teresia Mtewele akimuombea kura mgombea ubunge jimbo la Kalenga Jackson
Kiswaga ili aweze kushinda kwa kisindo katika uchaguzi wa mwaka
huu.
Na Fredy Mgunda, Iringa
MJUMBE wa halmashauri kuu ya taifa ya chama cha mapinduzi
(CCM) MNEC Teresia Mtewele amewaomba wananchi wa kata ya
Kihanga jimbo la Kalenga mkoani Iringa kuwachagua wagombea
wanaotokana na chama cha mapinduzi (CCM) kwa ajili ya kupata
maendeleo ya uhakika.
Akizungumza kwenye mkutano wa kuwanadi diwani na mgombea
ubunge wa jimbo hilo, Mtewele alisema kuwa wananchi
wanapaswa kuwachagua wagombea wa chama cha mapinduzi kwa
kuwa chama hicho ndio kinaweza kuleta maendeleo tofauti na
vyama vingine
Alisema kuwa chama cha mapinduzi kimejipanga kuhakikisha
kinaleta maendeleo katika kata ya Kihanga kwa kuwa tayari
wamejipanga kwa mikakati imara ya kufanya kazi za
kimaendeleo.
Mtewele alisema kuwa anajua kuwa kata hiyo wanakabiriwa na
changamoto ya ukosefu wa huduma za afya kwani hawana kituo
cha afya wala zahanati hivyo wakipewa ridhaa ya kuongoza
kata hizo watahakikisha wanatafuta ufunzi wa kero hiyo kwa
haraka.
"Najua kina mama wanajua kukiwa na tatizo kiafya hakuna
shughuli za kimaendeleo ambazo zitafanyika kwa urahisi hivyo
tupeni miaka mitano hii tuboreshe sekta ya afya kwa kuwa
viongozi wa CCM wamejipanga kutatua tatizo hilo,"alisema MNEC
Mtewele.
Aidha Mtewele alisema kuwa tatizo la maji kwenye baadhi ya
vijiji na vijiji vingine tatizo hill limetatuliwa kutokana
na kazi kubwa iliyofanywa na serikali ya awamu ya tano chini
ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Pombe
Magufulu.
Alisema kuwa wananchi wa Kihanga wanategemea kilimo kwa
kiasi kikubwa hivyo ni lazima kuwasaidia kupandisha thamani
ya mazao ili wakulima hao wapate faida ya kilimo hicho.
Mtewele alimazia kwa kuwaomba wananchi wa kata hiyo
kumchagua mgombea udiwani,ubunge na mgombea urais wa CCM kwa
kuwa hao ndio wanaweza kuleta maendeleo ya kweli kwa
wananchi wa kata na jumbo hilo.
Kwa upande wake mgombea ubunge wa jimbo la Kalenga kupitia
chama cha mapinduzi Jackson Kiswaga alisema kuwa atakuwa
kiongozi wa vitendo na sio maneno kama ilivyokuwa kwa
viongozi wengi hivyo wananchi wanapaswa kuchangua kwa kura
nyingi ili aweze kuwa mbunge wa jimbo hilo.
Kiswaga alisema kuwa wananchi wa kata ya kihanga wanabiliwa
na changamoto ya afya, mikopo ya kibiashara na elimu ya
ujasiliamali hivyo akipewa ridhaa ya kuwa mbunge wa jimbo
hilo atahakikisha anatatua changamoto hizo.
Aliwaomba wananchi wa kata hiyo kuhakikisha wanakipigia kura
zote kwa wagombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa ajili ya
maendeleo ya jimbo hilo na kata hiyo.
No comments:
Post a Comment